CHEKA UPUNGUZE 'STRESS'!!



Jumapili moja Mchagga kaingia kanisani kusali baada ya pilika za wiki nzima. Dakika chache likapitishwa kapu kwa ajili ya kutoa sadaka. Ilipofika zamu ya Mchagga, akachomoa noti ya Shilingi 500 na kuingiza kwenye kapu kwa kificho bila kuonekana na mtu yeyote jirani yake.
Baada ya dakika 15 hivi, Mchagga akahisi kuna mtu anamgusa begani kutokea benchi la nyuma yake. Akageuka na kumwona mzee mmoja wa makamo akimkabidhi noti mbili za Shilingi 10,000! Bila kusumbua akili, Mchagga akajua fika mzee yule anataka asaidiwe kuweka sadaka.
Akapokea na kuzitumbukiza ndani ya kapu. Baada ya misa kumalizika, Mchagga akamwendea yule mzee na kumpongeza, “Aisee, tunataka waumini kama wewe wenye moyo huo, yaani umechangia Shilingi 20,000! Sio jambo dogo mzee wangu, Mungu akubariki.”
Mzee akajibu, “Hapana, sijachangia mimi. Wakati unatoa sadaka yako mfukoni ndipo ukadondosha zile pesa. Nilichofanya ni kuziokota na kukurejeshea.” Kusikia vile Mchagga akamkimbilia Padri kuomba arejeshewe pesa zake, lakini akakataliwa kwa maelezo kwamba zimeshakabidhiwa kwa Mungu. Palepale akaanguka na kupoteza fahamu.
Alipozinduka akakutana uso kwa uso na mwanamke aliyevalia gauni jeupe. Mchagga akasema, “Afadhali nimekuona malaika, naomba umwambie Mungu anirejeshee zile pesa zangu!” Yule mwanamke akamjibu, “Mie sio malaika bali ni nesi. Walikuleta hapa hospitali ukiwa hujitambui!” Kusikia vile Mchagga akanguka na kupoteza tena fahamu…

No comments: