Chama
Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arusha, imesema chama hicho hakina mgombea
ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini, aliyeandaliwa hadi sasa.
Kimesema
mgombea mwenye sifa za kulikomboa jimbo
hilo, ambalo liko Chadema, hajajitokeza
mpaka sasa.
Akizungumza
na mwandishi hivi karibuni, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Arusha ,Feruzi Banno
alisema chama kina utaratibu wake wa
kampeni na chama hakina mgombea aliyeandaliwa kwa kuwa muda wa kuandaa wagombea
bado haujatangazwa.
Banno
alisema hayo alipotakiwa na gazeti hili, kufafanua kauli zilizozagaa jijini
Arusha kuwa
chama
hicho kimemwandaa mmoja wa wagombea (jina tunalo) ambaye yuko mstari wa mbele
kulitaka jimbo hilo kwa udi na uvumba na tayari ameanza harakati za kampeni kwa
kushirikiana na baadhi ya viongozi wa CCM kata, wilaya na mkoa.
Alisema
taarifa hizo zimekuwa zikisambazwa na wana CCM wenye kutaka ubunge Jimbo la
Arusha, ambao wanaoana kama wanatengwa.
Alisema
kura za maoni za kumsaka mgombea ubunge ndani ya chama, ndizo zitakazoamua na
si vinginevyo na kamwe chama hakitambeba mwana CCM .
Pamoja
na hayo yote, Katibu huyo alisema Jimbo
la Arusha lenye asilimia kuwa ya vijana, linahita mgombea mwenye kujichanganya
katika rika zote na anayekubalika bila ya kubabaisha, kwani huyo atafanya chama
kufanya kazi kwa urahisi na sio ngumu katika kampeni.
Banno
alisema kuwa CCM inahamu ya kulikomboa Jimbo la Arusha Mjini hivyo hatuhitaji
mgombea mzigo, ambaye itafika siku ya mwisho tukaanza kulaumiana hilo
halitakubalika kamwe kwa uongozi wa chama wilaya.
‘’Tunataka
mgombea kijana, mwenye kujichanganya katika vijiwe mbalimbali vya Jiji la Arusha na mwenye kujulikana katika kila
kona ya Jimbo la Arusha na mgombea huyo bado hajajitokeza hadharani. Hiyo
itasaidia chama kufanya kazi ndogo sana lakina hatutaki mgombea ambaye chama
kitafanya kazi ya ziada kumnadi, hilo halitakubalika kamwe. ‘’
Baadhi
ya wana CCM waliojitokeza na kuonesha nia ya kuwania ubunge Jimbo la Arusha
Mjini ni Kamanda wa Jumuiya ya Umoja wa
Vijana (UVCCM) Mkoa wa Arusha , Philemon
Mollel na Wakili wa Kujitegemea, Victor Njau.
Mwingine
ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Vijana Taifa, Dk Arod Adamson na Deo Mtui.
Wengine
wanaotajwa kuwania kiti hicho ni wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM ya wilaya ya
Arusha, mjumbe wa NEC Arusha, God
Mwalusamba, Mweka Hazina wa Chama wilaya ya Arusha Victor Mollel, Katibu
Mwenezi wa CCM wa wilaya ya Arusha, Gasper Kishimbua na Halima Mamuya.
Baadhi
ya wagombea hao tayari wengine wameshaanza kuchapisha fulana na kujitangaza
kuwa ni wateuliwe wa chama, wenye lengo la kukomboa jimbo hilo la Arusha Mjini,
hatua inayopingwa na chama ngazi ya Wilaya.
No comments:
Post a Comment