Mwili wa mtoto Yojana Bahati (1) ambaye
ana ulemavu wa ngozi (albino) umeokotwa msituni katika kijiji cha Ilelema.
Mtoto huyo alitekwa nyara juzi nyakati
za usiku na watu wasiojulikana mkoani Geita baada ya kumvamia nyumbani kwao
akiwa amelala na mama yake.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha
habari, mwili wa mtoto huyo ulikutwa ukiwa umefukiwa kwenye shamba moja
kijijini humo huku mikono na miguu yake ikiwa imekatwa na kunyofolewa.
Inasemekana wanakijiji wa Ilelema
wamekuwa wakikimbia huku na huko kujificha kwa kile kinachoaminika hofu ya
kukamatwa na vyombo vya dola kuhusiana na tukio hilo.
Taarifa za polisi zinasema kwamba
tayari mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na tukio hilo na kwamba anashikiliwa kwa
ajili ya mahojiano zaidi.
Katika tukio la kutekwa mtoto huyo,
mama wa albino huyo Ester (30) alijeruhiwa kwa kukatwakatwa kwa mapanga sehemu
mbalimbali za mwili na kisha watu hao kutokomea kusikojulikana.
No comments:
Post a Comment