Mkazi wa Bangulo Hali ya Hewa, Baraka Benson
(30) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, akikabiliwa na
mashitaka ya kumnajisi mtoto wa miaka minne.
Benson alifikishwa mahakamani hapo jana na
kusomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Hassan Juma.
Wakili wa Serikali, Florida Wenslaus alidai
kwamba Desemba 23 mwaka jana, maeneo ya Bangulo Hali ya Hewa Wilaya ya Ilala,
Benson alimnajisi mtoto huyo wa miaka minne kwa kumtia vidole sehemu za siri
huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Mshitakiwa alikana mashitaka na kurudishwa
rumande kwa kushindwa masharti ya dhamana.
Awali, wakili Wenslaus alidai kwamba upelelezi
wa kesi hiyo umekamilika na kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kumsomea
mshitakiwa maelezo ya awali.
Hakimu Juma alimtaka mshitakiwa kuwa na
wadhamini wawili ambapo mmoja kutoka taasisi inayotambulika, watakaosaini
dhamana ya Sh milioni mbili. Kesi itasikilizwa maelezo ya awali Machi 3 mwaka
huu.
Katika tukio jingine, mkazi wa Ubungo, Sad
Salimu (29) amepandishwa kizimbani katika mahakama ya mwanzo Kariakoo
akikabiliwa na mashitaka ya wizi wa vifaa vya umeme jua.
Karani Lucy Rutabanzibwa alidai kwamba Desemba
16 mwaka jana, maeneo ya mtaa wa Msimbazi na Masasi, Salimu aliiba vifaa 57 vya
umeme wa jua vyenye thamani ya Sh milioni 6.5 mali ya Kampuni ya Steps
Entertainment.
Mshitakiwa alikana mashitaka na kurudishwa
rumande kwa kushindwa masharti ya dhamana. Alitakiwa kuwa na wadhamini wawili
watakaosaini kulipa Sh milioni 3.5. Kesi itatajwa Machi 2 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment