Wabunge wanawake 19 wa Bunge la Tanzania wako
China katika ziara ya siku 11 yenye lengo la kubadilishana na kujifunza kwa
wenzao masuala ya uongozi na wanavyojihusisha kwenye shughuli za kijamii.
Akizungumzia ziara hiyo, Mwenyekiti wa Umoja
wa Wabunge Wanawake wa Bunge la
Tanzania, Anna Abdallah alisema moja ya malengo ya ziara yao wabunge hao ni kujifunza jinsi ya kuwajumuisha wanawake
kwenye uongozi.
"Mwaka huu ni wa uchaguzi na lazima
tuwaandae watakaogombea nafasi za uongozi, kwa hiyo hii ni ziara ya mafunzo ya
uongozi na kuangalia maendeleo, nia yetu kubwa ni kuona wenzetu jinsi
wanavyowasaidia wanawake kuondokana na umaskini," alisema.
Bunge la Tanzania lina asilimia 20 ya wabunge
wanawake na kwenye uchaguzi ujao huenda idadi ya wanawake ikaongezeka.
Makamu Mwenyekiti, Susan Limo alisema,
"Licha ya Beijing tutaenda Ghuanzhou, pia tutakutana na kundi la wabunge
wanawake wa China na naibu waziri anayeshughulikia masuala ya wanawake."
Anasema pia wakiwa hapa China, watajadili
masuala ya kuendeleza uchumi wa Tanzania kama vile sekta ya utalii na biashara.
Ziara hiyo ya wabunge wa Tanzania nchini China
ni sehemu ya mpango wa mabadilishano kati ya mabunge ya nchi hizo mbili.
Balozi wa Tanzania nchini China, Abdulrahman
Shimbo alisema, "tunategemea kwamba watakuza uhusiano haya na kwamba
wataweza kushirikiana katoka baadhi ya maeneo ya maendeleo na tunategemea zaidi
hasa kuwasaidia wanawake kwa upande wa elimu."
No comments:
Post a Comment