MUUZA SAMAKI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI


Mtu mmoja ameuawa na mwingine kujeruhiwa katika matukio mawili tofauti ya uhalifu yaliyotokea wilaya Bunda hivi karibuni.

Mfanyabiashara  wa samaki aliyeuawa kwa kupigwa risasi ni Mkome Marwa (39) mkazi wa mtaa wa Nyasura mjini Bunda.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Philipo Kalangi, tukio hilo ni la  Januari 12 mwaka huu saa 3:00 usiku katika eneo la Nyasura, mjini Bunda.
Marwa alikuwa na mkewe wakirejea nyumbani kwao kabla ya kupigwa risasi na  watu wasiofahamika. 
Kilangi alisema mauaji hayo, yana utata kwa kuwa walioua hawakuchukua chochote.
Katika tukio lingine la usiku huo wa Januari 12,  saa 4:00  eneo la Bunda Day, Ndaro Malemi (25), alijeruhiwa kwa  kupigwa risasi na mtu asiyefahamika ambaye pia hakuchukua kitu chochote. 
Akisimulia mkasa huo majeruhi huyo akiwa katika hospitali  ya DDH-Bunda, alisema kuwa mwanamume huyo aliyekuwa amevaa koti jeusi, alimvizia njiani na kumwamuru atoe kila kitu.
Alisema kwamba  alipojaribu kukimbia, ndipo mtu huyo alimpiga risasi mbili na kisha akatokomea kusikojulikana bila kuchukua kitu chochote.

No comments: