Shirika
la Maji Safi na Maji Taka jijini Dar es
Salaam (Dawasco) limezima mtambo wa Ruvu Juu kwa siku mbili, kutokana na kuwa
katika hali mbaya kwa muda mrefu, ikihitaji
kubadilishwa, jambo litakalosababisha baadhi ya maeneo kukosa huduma ya maji.
Ofisa
Uhusiano wa Shirika hilo, Eva
Lialo alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumzia ubadilishaji wa vifaa
hivyo katika mtambo huo na kuongeza kuwa marekebisho yalianza kufanyika tangu jana na
leo.
Alisema matengenezo hayo yamekuwa ya haraka na
dharura huku wakibadilisha vifaa vingine, ambavyo vilikuwa katika hali mbaya
kwa muda mrefu.
Alisema
pia katika marekebisho hayo, watabadilisha nguzo zinazoshikilia mita ambazo
zimelala sana na kuhatarisha usalama katika eneo husika.
"Kutokana
na hali hiyo Shirika litafanya matengenezo hayo kwa haraka kwa siku mbili
ambayo italazimu kuzima kabisa mtambo huo
kwa siku mbili kwa masaa saba hadi 10,” alisema Eva.
Alisema
kutokana na matengenezo hayo maeneo yafuatayo yatakosa maji kwa wakati huo
ambayo ni maeneo ya Kimara, Mbezi, Makuburi, External, Mlandizi,
Mburahati, Msewe, Changanyikeni na hata Kibamba.
No comments:
Post a Comment