Mtu
mmoja amekufa na wengine 21 kujeruhiwa, baada ya basi dogo aina ya Coaster walilokuwa
wakisafiria kutoka Shinyanga kwenye harusi, kurejea nyumbani kwao
Morogoro kupinduka katika kijiji cha Ikugha wilayani Ikungi kwenye barabara
kuu ya Singida - Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya
Singida, Queen Mlozi (pichani) akizungumza kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Singida, walikolazwa majeruhi, alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Jumamosi
iliyopita majira ya saa 8.00 mchana.
Alisema kuwa ajali
ilitokea baada ya Coaster hiyo, kuhamia upande wa kulia wa barabara, kukwepa
uharibifu uliotokana na kung’oka
mkanda wa chuma kwenye eneo hilo la
daraja, hivyo kusababisha kugongwa kwa nyuma na
basi la Zuberi lililokuwa
likipita kwa kasi.
Jina la dereva wa
basi hilo la Zuberi, lenye namba za usajili T 983 ABU, lililosababisha Coaster
hiyo kupoteza mwelekeo na kupinduka mara tatu, halijafahamika.
Jina la aliyekufa
kwenye ajali na majeruhi, hayakuweza kupatikana mara moja.
Ajali hiyo
imetokea kipindi ambacho kikosi cha usalama barabarani, kimeimarisha doria
sehemu mbalimbali nchini.
Walioshuhudia
ajali hiyo, walisema kuwa mwendo kasi na
uzembe wa madereva, bado ni kikwazo kwa usalama barabarani.
No comments:
Post a Comment