MDAU WA BLOGU YA ZIRO99 AAMUA KUCHANA NA UKAPERA...

Ilikuwa furaha, nderemo na vifijo!! Wakiwa na nyuso za furaha Bwana Elijah Eusebio Kitosi na Bi Upendo Deogratius Lufundya mara baada ya kufunga pingu za maisha kwenye Kanisa Katoliki la Maximillian Kolbe, Mwenge, Dar es Salaam Novemba 29, mwaka huu. Bwana harusi ni mwajiriwa wa kampuni ya Primefuels Ltd na Bi Harusi ni mwajiriwa wa Benki ya Posta.
Wakiwa wenye furaha, maharusi Elijah na Upendo pamoja na wapambe wao mara baada ya kufunga ndoa takatifu kwenye Kanisa Katoliki la Maximillian Kolbe-Mwenge, Dar es Salaam Novemba 29, mwaka huu. Watoto waliosimama mbele ni Thobias Mbagga na Celine Aggrey Kitosi.
Mdau wa blogu hii, Elijah Eusebio Kitosi akiwa mwenye furaha baada ya kukabidhiwa mke, Upendo Deogratius Lufundya wakati wa sherehe ya Send-Off iliyofanyika jijini Arusha Ijumaa ya Novemba 21, mwaka huu kwenye Ukumbi wa City Link.
Mzee Eusebio Kitosi, baba mzazi wa Elijah akitabasamu wakati wa sherehe ya Send-Off kwenye Ukumbi wa City Link, jijini Arusha Novemba 21, mwaka huu. Kulia ni mshenga, Bw David Koya.
Dada zake Elijah Eusebio Kitosi wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa sherehe ya Send-Off iliyofanyika Ijumaa ya Novemba 21, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Hoteli ya City Link, maeneo ya Phillips, jijini Arusha. Kutoka kulia ni Zitta Mgonja na Regia Fivawo. Kushoto ni Agnes Fivawo, mpwa wa Elijah.

No comments: