Mwendesha
pikipiki (bodaboda), mkazi wa Kitongoji cha Buriba katika mji mdogo wa
Sirari wilayani Tarime mkoani Mara, Mrimi Nyabikwi (23), amekutwa amekufa na
mwili wake kukutwa umening'inizwa kwenye mti maeneo ya Makaburini.
Kamanda wa Polisi
Tarime/Rorya, Lazaro Mambosasa amethibitisha kifo hicho. Alisema habari kutoka
ndani ya familia ya mtu huyo zilidai
kuwa Mrimi alitoweka nyumbani kwake kuanzia Desemba 24, mwaka huu.
Alisema marehemu
alikuwa amekodisha pikipiki ya mkazi wa Sirari kwa kufanyia kazi ya kusomba
abiria, lakini hakurejea nyumbani hadi mwili wake ulipokutwa na wachungaji wa
mifugo maeneo ya makaburi katika mji huo wa Sirari. Mwili wa mtu huyo ulikuwa
umeanza kuharibika.
Alisema kuwa mwili wa
mtu huyo, ulifanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Wilaya na kisha kukabidhiwa
kwa ndugu zake kwa maziko.
No comments:
Post a Comment