Upungufu wa vifaa vya kufundishia katika Shule ya Sekondari ya Wasioona ya Mvumi DCT iliyopo katika Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma unawakwamisha wanafunzi wasioona kufuata vyema na kwa wakati mtaala wa masomo.
Kauli
hiyo ilitolewa juzi na Mwalimu Mtaalamu wa shule ya wasioona ya Mvumi
DCT, Ernest Mbilu wakati wa ziara ya Balozi wa China nchini, Dk Lu Youqing.
Alisema
shule hiyo ina wanafunzi 31 wasioona ambapo wavulana ni 18 na wasichana ni 13
lakini wanafunzi hao wamekuwa wakichanganywa na wasioona..
Alisema
watoto wenye ulemavu wa kutoona wanahitaji kufundishwa kwa kutumia vifaa
maalumu ili waweze kwenda sambamba na wale wanaoona lakini upungufu wa vifaa
vya kufundishia wanafunzi wasiiona imekuwa ni kikwazo kikubwa.
Pia
mwalimu huyo alisema kama vifaa vya kufundishia wanafunzi wasioona vitapatikana
wanafunzi hao watafanya vizuri zaidi katika masomo yao tofauti na sasa ambapo
wamekuwa wakiachwa nyuma.
Akizungumza
na wanafunzi hao Balozi Youqing aliwataka kujifunza kwa bidii.
“Leo
mko darasani lakini kesho mtakuwa kwenye ujenzi wa nchi na mkitaka kuwa
wataalam na kupata maisha mazuri lazima kujifunza na kufanya kazi kwa bidii”
alisema
Pia
balozi huyo alisema Serikali ya China imetoa fedha kwa ajili ya kusaidia
shule hiyo na kati ya Sh milioni 50 zilizotolewa kusaidia elimu katika
Wilaya ya Chamwino, shule ya Mvumi wasioona DCT itapata sehemu yake katika
fedha hizo.
Aidha
balozi huyo alishiriki ujenzi wa maabara kwenye shule ya sekondari ya Mvumi.
Alisema
Tanzania ina raslimali nyingi ni vizuri kama watu wake wakaelimika na kupata
ujuzi mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa Taifa.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Fatma Ally alisema wilaya hiyo
inatakiwa kujenga vyumba 81 vya maabara.
Alisema
awali walitakiwa kukabidhi maabara hizo Novemba 15, mwaka huu lakini baada ya
kauli ya Rais Jakaya Kikwete kutaka kila shule kuwa na vyumba vitatu vya
maabara ana uhakika ifikapo Desemba 10, mwaka huu kazi hiyo itakuwa tayari.
Alisema
sasa vyumba vinne vya maabara vimekamilika, vyumba 25 viko katika hatua
mbalimbali lakini mpaka Desemba 10 watakuwa wamekamilisha agizo la Rais
Kikwete.
No comments:
Post a Comment