Shirika
la Usafiri Dar es Salaam (UDA) limezindua wiki ya huduma kwa wateja yenye kauli
mbiu ya ‘Safiri Salama’ ambayo mbali na mambo mengine lengo lake ni kuwawezesha
watumiaji wa usafiri huo kutoa maoni yao juu ya huduma zinazotolewa na shirika
hilo.
Katika
taarifa ya shirika iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari, Msemaji wake, George
Maziku alisema, huduma hiyo inayotarajiwa kumalizika Jumamosi wiki hii.
Itahusisha
wafanyakazi wao kutembelea maeneo mbalimbali, ikiwamo ndani ya mabasi ya
shirika hilo kwa lengo la kufahamu uhusiano kati ya makondakta, madereva na
wasafiri wa UDA.
Alisema
lengo jingine ni kuwawezesha wateja
wanaotumia mabasi ya kampuni hiyo kufahamu huduma zao, zikiwemo huduma za
kukodi mabasi na kutangaza biashara zao kupitia mabasi hayo.
Alisema
hiyo itatoa fursa ya wateja kutoa mapendekezo ya uboreshaji wa huduma zake na sekta nzima ya usafiri wa umma
jijini Dar es Salaam kwa ujumla.
Aliwataka
wateja kutumia kikamilifu fursa hiyo kwa kuongea bayana bila woga wowote
upungufu wa huduma zao, hususan tabia za madereva pamoja na makondakta kwa
lengo la kusaidia kuboresha zaidi huduma za shirika hilo.
Maziku
alisema kuwa wiki hii ya huduma kwa wateja, itatoa taswira halisi ya kufahamu
wateja wanapenda na wanataka nini kiboreshwe katika huduma za shirika hilo, na
pia itatoa picha ya kufahamu kuwa wateja wanaridhika au hawaridhiki na huduma
za shirika hilo.
Wiki
ya Huduma kwa Wateja ni wiki ya kimataifa ambayo huadhimishwa kuanzia Oktoba 6
mpaka 10, kila mwaka ambayo mashirika na makampuni mbalimbali huadhimisha kwa
kuwatembelea wateja wao kwa lengo la kusikia maoni yao.
No comments:
Post a Comment