Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajiwa wiki hii kuzindua
mradi wa sayansi na teknolojia wa elimu
ya juu katika vyuo vikuu mbalimbali nchini.
Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi, Profesa Sylvia Temo alisema jana kuwa mradi huo unaogharimu Dola za Marekani milioni 100 sawa na Sh
bilioni 165 ulianzishwa mwaka 2008 na kuisha Julai 31 mwaka huu.
Alisema ziara ya Waziri Mkuu itaanza leo, akianzia Chuo
Kikuu cha Sokoine (SUA) kilichopo mkoa wa Morogoro ambako atazindua miradi ya
majengo mbalimbali yakiwamo ya kilimo na biashara, masomo ya chakula na
teknolojia na uhandisi wa kilimo.
Kesho Waziri Pinda atatembelea Chuo Kikuu cha Dar es Saalam
(UDSM) na kuzindua mradi wa majengo
saba mapya na ukarabati
wa majengo matano katika chuo
hicho.
Alisema kupitia mradi
huo wameweza kuwasomesha walimu 120 kwa
Stashahada Uzamivu na Uzamili.
Kadhalika, Waziri Pinda atatembelea Chuo Kikuu Huria cha
Tanzania (OUT) na kufungua majengo yaliyojengwa kupitia mradi huo.
Profesa Temo aliongeza kuwa keshokutwa, Waziri Mkuu
atatembelea Chuo Kikuu Kishiriki cha
Elimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE)
ambapo atazindua jengo la kitaaluma la kuwaendeleza walimu na jengo
jipya la maabara ya kemia.
Alisema mradi huo ni miongoni mwa miradi mikubwa ambao
imeanzishawa tangu kuanza kwa uhuru hadi sasa.
“Mradi huo umeweza
kujenga majengo mapya 25, kurekebisha majengo, kusomesha walimu takriban 250,
kuboresha maabara, karakana na kuongeza
vifaa vya mafunzo,” alisema Profesa Temo.
Chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, mradi umetajwa kuboresha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama),
maktaba na pia kuboresha uongozi wa tasisisi mbalimbali za elimu na kuziunganisha
katika mtandao wa kitaifa.
Pia mradi huo umeboresha vyuo vikuu saba ambavyo ni Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kilichopo Morogoro, Chuo Kikuu cha Dar es
Saalam (UDSM), Chuo Kikuu Huria (OUT), Chuo Kikuu Ardhi na Chuo Kikuu Kishiriki
cha Elimu (Duce).
No comments:
Post a Comment