Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji
wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Tiba Asili ya Mwafrika yatakayofanyika
kuanzia Novemba 16, mwaka huu kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Maonesho hayo yatakayofanyika nchini
kwa mara ya kwanza yameandaliwa na Jukwaa la Tiba Asili Tanzania kwa
kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Mamlaka ya Maendeleo ya
Biashara Tanzania (Tantrade).
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati
ya Maandalizi ya Maonesho hayo, Boniventure Mwalongo, wadau mbalimbali wa tiba
asili na tiba mbadala wanatarajia kushiriki katika Maonesho hayo.
Mwalongo alisema washiriki hao ni
pamoja na watabibu wa tiba asili, watengenezaji wa dawa asili, wakunga wa tiba asili,
kampuni za dawa asili na vipodozi vya dawa asili, wasambazaji wa tiba
asili na tiba mbadala, watengenezaji wa vyakula asili, kliniki za tiba asili na
tiba mbadala.
Aidha, Mwalongo alisema wanaendelea
na taratibu za kufanya maongezi na wadhamini mbalimbali ambapo watatoa taarifa
rasmi baada ya kufikia tamati ya maongezi, ikiwa ni pamoja na kutoa ratiba
nzima ya maonesho hayo. Wadau wasiopungua 280
wameonesha nia ya kushiriki.
No comments:
Post a Comment