Mkuu wa Uchunguzi wa Maandishi
wa Jeshi la Polisi Kenya, John Kimani ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
jijini Dar es Salaam kuwa saini zinazodaiwa kusainiwa na Ramadhani Balenga
katika hati ya uhamishaji umiliki wa kiwanja pamoja na mkataba wa mauziano ni
za kughushi.
Kimani alidai hayo katika mahakama
hiyo wakati akitoa ushahidi katika kesi ya kughushi inayomkabili Mkurugenzi wa
Hoteli ya Rick Hill, Hans Macha.
Katika kesi hiyo,
mfanyabiashara huyo anakabiliwa na mashitaka ya kughushi hati ya kiwanja chenye
namba 183, Block A kilichopo Kigogo.
Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu
Mkazi, Devotha Kisoka, Kimani alidai alifanya uchunguzi baada ya Polisi nchini
kumpelekea nyaraka, ikiwemo mkataba wa mauziano na nyaraka za uhamishaji
umiliki wa kiwanja kwa ajili ya kuzifanyia uchunguzi.
Aliieleza mahakama kuwa baada
ya uchunguzi wao uliotumia vifaa vya utaalamu, walibaini kuwa saini zilizopo
kwenye nyaraka hizo siyo za Balenga ni za kughushi.
Alidai wakati wanafanya
uchunguzi walizingatia mambo mengi ikiwamo kuangalia mgandamizo wa kalamu,
saini zote zilizokuwa na utata kwa kutumia kifaa maalumu.
Katika hatua nyingine,
mpelelezi wa kesi hiyo, Inspekta Lugano Mwampeta alisema aliwahoji watu
mbalimbali kuhusu jalada hilo, akiwemo Msajili wa Hati katika Ofisi ya Wizara
ya Ardhi, na kubaini hati hiyo ina utata katika saini.
Aidha, alisema alifika katika
eneo la kiwanja hicho ambacho kimejengwa ghorofa, na kugundua jengo hilo
haliwezi kuuzwa kwa Sh milioni 20.
Hakimu Devotha, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 6,
mwaka huu kwa ajili ya kuendelea kusikiliza ushindi wa upande wa Jamhuri.
No comments:
Post a Comment