Siti, binti wa
Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu, usiku wa kuamkia leo ameibuka kidedea katika
kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Tanzania
(Redd’s Miss Tanzania 2014) katika shindano lililofanyika kwenye Ukumbi
wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Mlimbwende
huyo, ambaye kablaya kutwaa taji hilo alitawazwa kuwa Miss Temeke, aliwabwaga
warembo wengine 30 waliokuwa wakiwania taji hilo mwaka huu.
Kwa ushindi
huo, Siti amejinyakulia kitita cha Shilingi milioni 18, ambapo ukumbini hapo
alikabidhiwa hundi ya thamani ya Shilingi milioni 10 kwa maelezo kwamba kiasi
kilichobaki cha Shilingi milioni 8 atakabidhiwa baada ya shindano hilo.
Siti
ataiwakilisha Tanzania kwenye shindano la Miss World mwakani, ambapo mwaka huu
Tanzania itawakilishwa na mshindi wa mwaka jana, Happiness Watimanywa kutoka
Dodoma.
No comments:
Post a Comment