Watu
wawili wamekufa na wengine watano kujeruhiwa baada ya magari mawili, likiwamo
basi dogo la abiria walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori la
mafuta.
Kwa
mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Athuman Mwambalaswa alisema
kuwa tukio hilo lilihusisha gari aina ya Toyota Coaster lililokuwa linatokea
kwenye msiba Musoma mkoani Mara kwenda Dar es Salaam na kugongana na lori la
mafuta.
Kamanda
Mwambalaswa alisema kuwa ajali hiyo ilitokea juzi maeneo ya Ubena Senge katika
barabara ya Morogoro, chanzo kikitajwa kuwa ni uzembe wa gari dogo aliyehama
upande wake kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni uchovu wa safari ndefu.
Alisema
basi dogo lenye namba za usajili namba T 663 BKP lililokuwa likiendeshwa na
Ally Abdul (34), likiwa na abiria 20 liligongana na lori la mafuta aina ya
Leyland Daf lenye namba za usajili T 858 CLK na tela namba T 421 CKY, mali ya
kampuni ya Ramader ya Dar es Salaam ambalo dereva wake ametajwa kwa jina moja
la Rashid.
Aliwataja waliokufa kwenye ajali hiyo kuwa
ni Neema Mile (39) na Jane Mtani (38) ambao miili yao imehifadhiwa katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani, Tumbi ambako pia majeruhi wamelazwa.
No comments:
Post a Comment