Pingamizi
la Mwanasheria Mkuu (AG) dhidi ya ombi la kibali cha kufungua kesi ya kupinga
vikao vya Bunge Maalumu la Katiba vinavyoendelea mkoani Dodoma limetupiliwa
mbali katika
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam.
Pingamizi hilo lilikuwa la
kupinga ombi lililowasilishwa na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS)
waliofungua kesi ya kikatiba wakiomba mahakama itoe zuio la kuendelea kwa vikao
vya Bunge maalumu la katiba hadi kesi hiyo itakapokwisha.Aidha, wanaomba Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) awasilishe bungeni muswada wa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba namba 8 ya mwaka 2011 na namba 2 ya
mwaka 2012, sura ya 83 na
ifafanue kifungu cha 25 cha sheria hiyo.
Uamuzi huo ulitolewa jana na
jopo la majaji watatu wanaosikiliza ombi hilo wakiongozwa na Jaji Augustine
Mwarija, Dk Fauz Twaib na Aloyisius Mujulizi.
Wakati huo huo, kesi nyingine
ya kikatiba iliyofunguliwa na Mwandishi wa Habari, Saidi Kubenea akihoji
mamlaka ya Bunge hilo inaanza kusikilizwa leo ambapo ilitakiwa ianze
kusikilizwa jana lakini AG aliwasilisha pingamizi ambalo pia litaendelea
kusikilizwa leo.
Katika kesi hiyo, Kubenea
anaiomba mahakama hiyo itoe tafsiri sahihi ya Mamlaka ya Bunge la Katiba, kwa
kuzingatia kifungu cha 25 (1) na (2) cha Sheria ya Mbadiliko ya Katiba namba 83
ya mwaka 2011.
Aidha, anaiomba mahakama
itamke kama bunge hilo lina mamlaka ya kubadilisha maudhui ya Rasimu ya Katiba
iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kwa kiwango gani.
No comments:
Post a Comment