Mwanamke
anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 25 amekufa papo hapo baada ya kudondoka
kwenye pikipiki aliyokuwa amepanda na kisha kukanyagwa na gari.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema kuwa ajali hiyo ilitokea
juzi mchana katika barabara ya Bagamoyo eneo la Tangibovu ambapo gari
likiendeshwa na dereva asiyefahamika akitoka kwa Alysykes kuingia barabara ya
Bagamoyo, aliigonga pikipiki namba T 505 CTJ Fekon ikiendeshwa na dereva asiyefahamika.
Alisema
pikipiki hiyo iliyokuwa ikitokea Mbezi Makonde kwenda Mwenge ilikuwa imempakia
mwanamke huyo ambaye baada ya pikipiki kugongwa alianguka chini na kisha
kukanyagwa na lori namba T 277 CIL aina ya Tata likiwa na trela namba T 339 CYB
lililokuwa katika uelekeo mmoja na pikipiki.
Kamanda
alisema mwanamke huyo alikufa papo hapo na mwili wake umehifadhiwa katika
Hospitali ya Mwananyamala huku Polisi wakiendelea kuwasaka madereva waliohusika
katika ajali hiyo.
Wakati
huo huo moto umezuka katika baa ya Elements iliyopo maeneo ya Masaki na
kuteketeza eneo la jikoni na mali zote zilizokuwamo ndani. Thamani bado
haijajulikana na haukuwa na madhara kwa binadamu.
No comments:
Post a Comment