Katika
hali isiyotarajiwa, mwanafunzi wa Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari ya
Wavulana Ihungo Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, Ezra Gerald (19), amejinyonga
hadi kufa kwa kutumia shuka ya hospitali, alikokuwa amelazwa kwa kile kinachoeleza
alikuwa anasumbuliwa na homa ya matumbo.
Hata
hivyo, ujumbe ulioachwa na marehemu huyo unaonesha alichukua uamuzi huo,
kutokana na kuchukizwa na uamuzi wa daktari aliyemhudumia wa kumlaza ili
atibiwe ugonjwa ambao hakuwa anaumwa.
Aidha,
katika ujumbe huo imeelezwa alichukizwa na kitendo cha kupotezewa muda
hospitalini wakati wenzake wakiendelea na masomo.
Tukio
hilo limethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Gilles Muroto
aliyesema mwanafunzi huo alijinyonga Septemba 16 mwaka huu saa moja asubuhi.
Alisema
mwili wake uligundulika ukining’inia kwenye mti uliopo maeneo ya hospitali hiyo
na alipopekuliwa katika mifuko ya suruali yake, zilionekana karatasi mbili,
moja ikiwa na ujumbe uliosomeka; “Haiwezekani binadamu kuhudumiwa kama mbwa,
yaani nafika hospitali najieleza hali yangu halafu daktari ananiandikia kulazwa
bila kupima, sasa sijui wanatibu nini?
“Kwa
kweli siwezi kuvumilia wenzangu wanasoma halafu mimi nimekalishwa tu hapa
hospitali bila kujua wananitibu nini, inaniuma sana mpaka nafikia hatua hii ya
kujiondoa duniani kwa sababu naona watu wanachezea ndoto zangu, mimi siwezi
kuona ndoto yangu inazimwa wakati natakiwa niwepo shuleni nikamilishe ndoto
zangu “mjitahidi tukutane mbinguni “Respect My Family and Brother Henry.”
Kamanda
Muroto amesema hakuna aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo, lakini polisi
wanaendelea na uchunguzi.
Inaelezwa
mwanafunzi huyo aliyetajwa kuwa ni mwenyeji wa mkoa wa Tabora, alilazwa
hospitalini hapo tangu Septemba 11 mwaka huu.
Kwa
mujibu wa Katibu wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera, Benges Justus, tukio hilo
lilitokea Septemba 16, mwaka huu, siku moja baada ya mgonjwa huyo kulazwa.
Alisema baada ya mwanafunzi huyo kupokelewa
hospitalini hapo, alifanyiwa vipimo vyote vya kitabibu na kugundulika
anasumbuliwa na malaria, ndipo akaanzishiwa tiba ya ugonjwa huo.
No comments:
Post a Comment