Kesi ya
aliyejifanya askari polisi wa usalama barabarani, James Hassan (45) imeendelea
kupigwa kalenda kutokana na mshitakiwa kutofika mahakamani hapo licha ya kuwepo
kwa mashahidi wawili.
Kesi hiyo
iliyofikia hatua ya kusikilizwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imekuwa
ikipigwa kalenda mara kwa mara kutokana na mshitakiwa huyo kudai kwamba anaumwa
hivyo kukwamisha kesi hiyo kuendelea.
Wakili wa
Serikali, Felista Mosha alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Hassan Juma
kwamba mashahidi wawili wamefika mahakamani hapo kwa ajili ya kutoa ushahidi
wao lakini kutokana na mshitakiwa kuwa mgonjwa, aliomba tarehe nyingine ya
kusikiliza shauri hilo.
Hakimu Juma
alikubaliana na ombi hilo na kuahirisha shauri hilo hadi Septemba 24, mwaka huu
kwa hatua za usikilizwaji.
Shahidi wa
pili katika kesi hiyo aliieleza Mahakama jinsi mshitakiwa alivyojipatia sare za
askari polisi kutoka kwa marehemu baba yake mdogo na kujifanya askari wa
usalama barabarani.
Mshitakiwa
huyo alifikishwa mahakamani Agosti 14, mwaka jana, kujibu mashitaka ya
kujifanya askari polisi baada ya kukutwa Kinyerezi Mnara wa Voda na kukana
mashitaka hayo. Yupo rumande.
No comments:
Post a Comment