Mahakama
ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kifungo cha miaka 15 jela, Hassan Suleiman (23)
mkazi wa Kitunda, kwa kupatikana na hatia ya kumdhalilisha mtoto wa miaka
mitatu kwa kumchezea sehemu zake za siri kwa vidole.
Akisoma
hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi Mwandamizi, Hassani Juma alisema kuwa mshitakiwa
huyo atatumikia kifungo hicho iwe fundisho kwa wengine.
Pia
Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa
mahakamani hapo kutumia mashahidi wanne ikiwamo mtoto aliyefanyiwa vitendo
hivyo pamoja na ushahidi wa fomu ya Polisi ya Matibabu (PF3) iliyotolewa
mahakamani hapo kama kielelezo.
Awali,
Wakili wa Serikali, Felista Mosha alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo Oktoba
23, mwaka jana, maeneo ya Kitunda Migombani wilayani Ilala ambapo alimwingizia
vidole sehemu za siri mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa shule ya awali
ya Kitunda Mwanagati, wilayani
humo.
Katika
utetezi wa awali alioutoa mshitakiwa, alidai mtoto huyo alipotea baada ya
kutoka shuleni na kwenda nyumbani kwake kuomba maji ya kunywa ndipo alimueleza
Suleiman kwamba amsaidie kumpeleka nyumbani kwao ambako hata yeye mwenyewe
hakujui.
No comments:
Post a Comment