Matumizi ya
dawa za kienyeji kwa ajili ya kuongeza uchungu na kujifungua mapema, imeelezwa
kuchangia zaidi vifo kwa wajawazito.
Mganga Mkuu
wa Mkoa Kigoma, Dk Leonald Subi alisema hayo mjini Kigoma kwenye kikao cha
wadau wa afya.
Kikao hicho
kilihusisha kufanya tathmini na kuona hatua za kuchukua kukabiliana na vifo vya
wajawazito na watoto wakati wa kujifungua mkoani humo. Kiliitishwa na shirika
la Wolrd Lung Foundation.
Dk Subi
alisema kuwa licha ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali kwa
kushirikiana na wadau wengine, kukabiliana na hali hiyo, bado wajawazito
wanajifungulia majumbani na kutumia dawa hizo hatarishi kwa maisha yao.
Alisema
kumekuwa na upungufu wa vifo vya wajawazito na ongezeko la vifo vya watoto.
Alisema vifo
vya wajawazito vimepungua kutoka vifo 74 mwaka 2009 hadi kufikia 49 kwa mwaka
jana huku vifo vya watoto wachanga vikiongezeka kutoka 720 mwaka 2009 na
kufikia 840 mwaka jana.
Mkurugenzi wa
Miradi wa World Lung Foundation, Dk Nguke Mwakatundu alisema shirika lake
linaboresha huduma za mama na mtoto mkoani humo, lakini changamoto ya vifo vya
wajawazito ni kubwa, kutokana na kujifungulia majumbani.
No comments:
Post a Comment