Ajali nyingine imetokea nchini na safari hii imehusisha basi
la Air Bus lililokuwa likitoka Dar es
Salaam kwenda Tabora.
Ajali hiyo iliyotokea mkoani Morogoro jana,
ilisababisha vifo vya watu wanne na
majeruhi wapatao 35.
Imetokea siku chache tangu ajali ya hivi karibuni iliyoua
watu 39, iliyohusisha magari matatu wilayani Butiama, Mkoa wa Mara.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul alisema
ajali hiyo ilitokea jana saa 5: 45 asubuhi
katika eneo la Daraja la Mkange kati ya Kijiji cha Berega na Kiegeya
wilayani Kilosa.
Waliopoteza maisha ni wanawake watatu na mwanamume, ambao walikufa papo hapo na majina yao
hayakupatikana. Majeruhi walikimbizwa
Hospitali ya Misheni ya Berega.
Kamanda alisema
basi hilo lenye namba za usajili
T106 AGB, lilikuwa likitoka Dar es Salaam kwenda mkoani Tabora.
Alisema kutokana na mwendo kasi, liliacha njia na kwenda kutumbukia korongoni kwenye
daraja la Mkange lililopo kwenye
barabara kuu ya Morogoro- Dodoma.
Dereva wa basi hilo, Bilal Seif alitoweka eneo hilo na Polisi inamsaka achukuliwe hatua
za kisheria.
Mganga wa zamu wa Hospitali ya Misheni ya Berega wilaya ya
Kilosa, Alfred Chiponda, alisema kati ya majeruhi, 10 ni wanawake, sita ni watoto na 19 ni wanaume ambao wameumia vibaya kwa kuvunjika
sehemu mbalimbali mwilini.
Walioumia vibaya wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Morogoro.
Mashuhuda wa ajali hiyo, walisema dereva wa basi hilo alikuwa kwenye mwendo kasi na alitaka kupita
gari lingine, lililokuwa mbele yake na kupoteza mwelekeo, hali iliyosababisha
gari hilo kuacha njia na kupinduka eneo
la darajani.
No comments:
Post a Comment