Mkazi wa
Kijiji cha Bupu wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani, Forodesi Ntabegera (30)
ameuawa kwa kubakwa, kisha kunyongwa na watu wasiojulikana, kisha mwili wake
kutupwa kichakani.
Kaimu Kamanda
wa Polisi mkoa wa Pwani, Athuman Mwambalaswa alieleza kuwa Ntabegera alinyongwa
na watu hao kwa kutumia kitenge chake alichovaa.
Mwambalaswa
alisema Septemba 9 mwaka huu saa 8:00 mchana wakazi wa kijiji hicho, walifanya
msako wa kumtafuta Ntabegera baada ya kupotea Septemba 8 mwaka huu.
“Baada ya
msako huo kufanyika, mwili wa marehemu ulikutwa kwenye kichaka umbali wa mita
30 kutoka barabarani, ambapo mwili wake ulimwagiwa unga kichwani na mgongoni,”
alisema Kamanda.
Kamanda
alisema wauaji walitumia mfuko aliobebea unga Ntabegera akitokea kusaga,
kumvisha miguuni kisha mwili wake waliulaza kifudifudi. Polisi inawasaka
wahusika.
No comments:
Post a Comment