Wavuvi tisa wakazi wa kijiji cha uvuvi cha Mpasa wilayani Nkasi mkoa wa Rukwa, wamekufa baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Tanganyika.
Habari kutoka eneo la tukio, ambazo pia zimethibitishwa na jeshi la polisi, zinasema wavuvi hao walikuwa wakisafiri kwenda katika Mji wa Mpulungu, mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika nchi jirani ya Zanmbia. Walikuwa wakitokea kijiji cha uvuvi cha Mpasa wilayani Nkasi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Ferdinand Rwegasira, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Alisema miili yote tisa ya waliokuwa wakisafiri ndani ya boti hiyo, haijapatikana hadi sasa.
Alitaja wanaosadikiwa kufa ni Fadhili Nkambi (30), Shaaban Kasokota ((33) Audifas Miele (43), Linus Maliyatabu (38), Kashindi Tantika (25), Venus Albeto (35), Geofrey Kazumba (24), Mwambe Ntapantapa (21) na Mathias Ulaya (20) .
Kamanda Rwegasira alisema uchunguzi wa ajali hiyo ya majini, bado unaendelea na pia wanaendelea kutafuta miili hiyo.
Akizungumza na mwandishi kwa simu kutokea eneo la tukio, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kasanga mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo, Francis Simfukwe alisema wavuvi hao walianza safari yao kuelekea Zambia Julai 28 mwaka huu sasa 11:00 alfajiri .
Alisema wavuvi hao walikuwa wakisafiri kwenda mji wa Mpulungu, Zambia kuuza samaki wao, waliowavua kwa ndoano na kuwahifadhi katika makasha 27, ambapo kila mvuvi alikuwa na makasha matatu .
“Sasa kwa kuwa walikuwa wakikwepa kupitia kijijini Kasanga ili wasiweze kulipa ushuru wa samaki hao, waliokuwa wakisafirishwa kwenda nchi jirani ya Zambia, walipita nchi jirani ya Kongo ( DRC) katika Ziwa, hivyo kufanikiwa kukwepa kupita katika kijiji cha Kasanga ambayo ni bandari ya mwisho katika Ziwa Tanganyika kwa upande wa Tanzania kabla ya kuingia nchini Zambia,” alidai Simfukwe.
Kwa mujibu wa Simfukwe, wavuvi hao walipofika vijiji vya uvuvi vya Kilewani na Kipwa mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo, ghafla upepo mkali ulivuma ndipo walipoamua kuanza kurejea ufukweni mwa kijiji cha uvuvi cha Kipwa. Lakini, boti yao ilipigwa na dhoruba kali na kuzama.
“Siku iliyofuata makasha manne yakiwa na samaki wabichi, huku yakiwa yameandikwa majina, yalionekana yakielea ziwani katika kijiji cha Kipwa…ndipo tulipohisi kuwa kuna ajali imetokea ziwani," alieleza Simfukwe.
Simfukwe alisema wakazi wa kijiji cha uvuvi cha Nsumba mwambao mwa Ziwa Tanganyika nchini Zambia, walitoa taarifa kuwa wameona mtumbwi ukielea ziwani, karibu na kijijini chao ukiwa hauna wala mashine ya kuendeshea.
Baadhi ya wavuvi wa kijiji cha Mpasa, walimweleza mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, kwa masharti ya kutoandikwa majina yao, kuwa baada ya kukatika kwa mawasiliano ya simu baina yao na wavuvi wenzao, waliokuwa wakisafiri kwa boti kuelekea nchini Zambia kuuza samaki wabichi, walianza kuwatafuta .
Habari kutoka eneo la tukio, ambazo pia zimethibitishwa na jeshi la polisi, zinasema wavuvi hao walikuwa wakisafiri kwenda katika Mji wa Mpulungu, mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika nchi jirani ya Zanmbia. Walikuwa wakitokea kijiji cha uvuvi cha Mpasa wilayani Nkasi.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Ferdinand Rwegasira, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Alisema miili yote tisa ya waliokuwa wakisafiri ndani ya boti hiyo, haijapatikana hadi sasa.
Alitaja wanaosadikiwa kufa ni Fadhili Nkambi (30), Shaaban Kasokota ((33) Audifas Miele (43), Linus Maliyatabu (38), Kashindi Tantika (25), Venus Albeto (35), Geofrey Kazumba (24), Mwambe Ntapantapa (21) na Mathias Ulaya (20) .
Kamanda Rwegasira alisema uchunguzi wa ajali hiyo ya majini, bado unaendelea na pia wanaendelea kutafuta miili hiyo.
Akizungumza na mwandishi kwa simu kutokea eneo la tukio, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kasanga mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo, Francis Simfukwe alisema wavuvi hao walianza safari yao kuelekea Zambia Julai 28 mwaka huu sasa 11:00 alfajiri .
Alisema wavuvi hao walikuwa wakisafiri kwenda mji wa Mpulungu, Zambia kuuza samaki wao, waliowavua kwa ndoano na kuwahifadhi katika makasha 27, ambapo kila mvuvi alikuwa na makasha matatu .
“Sasa kwa kuwa walikuwa wakikwepa kupitia kijijini Kasanga ili wasiweze kulipa ushuru wa samaki hao, waliokuwa wakisafirishwa kwenda nchi jirani ya Zambia, walipita nchi jirani ya Kongo ( DRC) katika Ziwa, hivyo kufanikiwa kukwepa kupita katika kijiji cha Kasanga ambayo ni bandari ya mwisho katika Ziwa Tanganyika kwa upande wa Tanzania kabla ya kuingia nchini Zambia,” alidai Simfukwe.
Kwa mujibu wa Simfukwe, wavuvi hao walipofika vijiji vya uvuvi vya Kilewani na Kipwa mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo, ghafla upepo mkali ulivuma ndipo walipoamua kuanza kurejea ufukweni mwa kijiji cha uvuvi cha Kipwa. Lakini, boti yao ilipigwa na dhoruba kali na kuzama.
“Siku iliyofuata makasha manne yakiwa na samaki wabichi, huku yakiwa yameandikwa majina, yalionekana yakielea ziwani katika kijiji cha Kipwa…ndipo tulipohisi kuwa kuna ajali imetokea ziwani," alieleza Simfukwe.
Simfukwe alisema wakazi wa kijiji cha uvuvi cha Nsumba mwambao mwa Ziwa Tanganyika nchini Zambia, walitoa taarifa kuwa wameona mtumbwi ukielea ziwani, karibu na kijijini chao ukiwa hauna wala mashine ya kuendeshea.
Baadhi ya wavuvi wa kijiji cha Mpasa, walimweleza mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, kwa masharti ya kutoandikwa majina yao, kuwa baada ya kukatika kwa mawasiliano ya simu baina yao na wavuvi wenzao, waliokuwa wakisafiri kwa boti kuelekea nchini Zambia kuuza samaki wabichi, walianza kuwatafuta .
No comments:
Post a Comment