WAJASIRIAMALI WAANDALIWA KONGAMANO



Kampuni ya Food Safety and Quality Consultancy imeandaa makongamano kwa ajili ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo na wa kati waweze kuyafikia masoko bora ya kimataifa.
Ofisa Mtendaji wa kampuni hiyo, Paul Seni alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa.
Alisema makongamano hayo yatafanyika Mwanza, Agosti 25 na 26 na jijini Dar es Salaam Agosti 28 na 29 mwaka huu.
Alisema kampuni hiyo iliyosajiliwa na Serikali mwaka 2013, ilianzishwa kwa lengo la kuwashirikisha wajasiriamali wa Tanzania  waweze kuzalisha bidhaa bora kuhimili ushindani wa masoko na kuongeza kipato chao kwa kutumia fursa zinazowazunguka ndani na nje ya nchi.
Seni alisema mafunzo hayo yatahimiza ubora wa vyakula kuanzia utayarishaji shamba, matumizi mazuri ya virutubishi bora kama mbolea, viuagugu, viuatilifu, viua dudu na namna ya kuondoa visumbufu vinavyoharibu ubora wa mazao shambani, ghalani, katika usindikaji na uhifadhi bora wa mazao.
Pia kampuni hii inajenga uwezo kwa wajasiriamali wanaomiliki biashara ya vyakula kwa wenye mahoteli, migahawa au wasindikaji hafifu wa vyakula kuongeza ubora na kuondoa magonjwa yanayoletwa na utayarishaji hafifu wa vyakula.

No comments: