MKATABA KUSAIDIA MAENDELEO YA UMEME WASAINIWA


Serikali imesaini makubaliano na Marekani kwa ajili ya kutekeleza mpango wa nchi hiyo kusaidia maendeleo katika Sekta ya Umeme.
Waziri wa Nishati na Madini,  Profesa Sospeter Muhongo pamoja na Balozi wa Marekani nchini,  Mark  Childress walisaini Makubaliano ya Awali juzi katika Ubalozi wa Tanzania Washington DC, Marekani.
Mpango huo wa Marekani kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya Sekta ya Umeme Afrika ujulikanao kama ‘Power Africa Initiative’, umetengewa Dola za Marekani bilioni saba na serikali ya nchi hiyo.
Kampuni binafsi za nchi hiyo ziliahidi kuwekeza Dola za Marekani bilioni tisa 9.
Mpango huo uliozinduliwa na Rais Barack Obama wa Marekani alipotembelea  nchini Julai mwaka jana. Utainufaisha Tanzania pamoja na nchi nyingine zikiwemo   Ethiopia, Ghana, Nigeria, Liberia na Kenya.
Hafla hiyo pia  ilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Liberata Mulamula.

No comments: