Idara ya afya mkoani hapa imehadharisha jamii dhidi ya ugonjwa wa ini, ikisema ni mbaya zaidi ya virusi vya Ukimwi.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Emmanuel Mtika alitoa hadhari hiyo kwenye kikao cha 27 cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), mwishoni mwa wiki mjini hapa.
Alikuwa akiwasilisha taarifa ya hali ya upatikanaji wa damu salama katika vituo, vinavyotoa huduma ya afya mkoani humo.
Alisema virusi vya homa ya ini viligunduliwa kwenye damu, iliyokusanywa kutoka kwa watu wanaochangia damu kwa hiari yao, kuokoa maisha ya wahitaji wakiwemo wajawazito na watoto.
“Idara ya Afya imekumbana na changamoto kubwa ya magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya damu hususani homa ya ini, kama iliyogunduliwa kutoka kwenye damu iliyokusanywa kutoka kwa wateja,” alisema.
Alisema magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya damu yaliyogundulika kwenye damu iliyokusanywa ni homa ya ini aina ya HBV.
Kwa mujibu wake, asilimia 10.3 ya watu 206 waliopimwa walikutwa na maambukizi ya aina hiyo HBV, wakati aina nyingine ya homa ya ini ya HCV ambapo ni asilimia 1.5 ya watu 30 walikutwa na maambukizi ya ugonjwa huo.
Kwa upande wa maambukizi ya virusi vya Ukimwi, ni asilimia 1.2 ya watu 28 waliopimwa na kukutwa na maambukizi hayo.
Akitoa mfano wa upatikanaji hafifu wa damu salama katika vituo vinavyotoa huduma ya afya mkoani humo, alisema mahitaji ni chupa za damu 4,350 kwa mwaka. Lakini, ni chupa 2,003 tu zilizokusanywa mwaka jana, ambazo ni sawa na asilimia 53 ya mahitaji halisi.
“Hata hivyo ni chupa za damu zipatazo 1,665 tu zilizosambazwa katika vituo vitano vinavyotoa huduma ya afya mkoani kwetu…hiki ni kiwango kidogo sana ikilinganishwa na mahitaji halisi,” alisema.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Emmanuel Mtika alitoa hadhari hiyo kwenye kikao cha 27 cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), mwishoni mwa wiki mjini hapa.
Alikuwa akiwasilisha taarifa ya hali ya upatikanaji wa damu salama katika vituo, vinavyotoa huduma ya afya mkoani humo.
Alisema virusi vya homa ya ini viligunduliwa kwenye damu, iliyokusanywa kutoka kwa watu wanaochangia damu kwa hiari yao, kuokoa maisha ya wahitaji wakiwemo wajawazito na watoto.
“Idara ya Afya imekumbana na changamoto kubwa ya magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya damu hususani homa ya ini, kama iliyogunduliwa kutoka kwenye damu iliyokusanywa kutoka kwa wateja,” alisema.
Alisema magonjwa yanayoambukizwa kwa njia ya damu yaliyogundulika kwenye damu iliyokusanywa ni homa ya ini aina ya HBV.
Kwa mujibu wake, asilimia 10.3 ya watu 206 waliopimwa walikutwa na maambukizi ya aina hiyo HBV, wakati aina nyingine ya homa ya ini ya HCV ambapo ni asilimia 1.5 ya watu 30 walikutwa na maambukizi ya ugonjwa huo.
Kwa upande wa maambukizi ya virusi vya Ukimwi, ni asilimia 1.2 ya watu 28 waliopimwa na kukutwa na maambukizi hayo.
Akitoa mfano wa upatikanaji hafifu wa damu salama katika vituo vinavyotoa huduma ya afya mkoani humo, alisema mahitaji ni chupa za damu 4,350 kwa mwaka. Lakini, ni chupa 2,003 tu zilizokusanywa mwaka jana, ambazo ni sawa na asilimia 53 ya mahitaji halisi.
“Hata hivyo ni chupa za damu zipatazo 1,665 tu zilizosambazwa katika vituo vitano vinavyotoa huduma ya afya mkoani kwetu…hiki ni kiwango kidogo sana ikilinganishwa na mahitaji halisi,” alisema.
No comments:
Post a Comment