Dereva wa basi lililotumbukia katika korongo na kuua watu sita na kujeruhi vibaya wengine 18, waliokuwa wakisafiri kutoka Mbinga mjini kwenda Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, amejisalimisha polisi akiwa katika hali mbaya.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela amemtaja dereva huyo ni Paul Nchimbi (31), mkazi wa kijiji cha Liparamba wilayani Nyasa.
Kamanda alisema mwili wa dereva huyo, umejaa majeraha na kwa kuwa amepatikana kwa hiari yake na kuripoti katika kituo kikuu cha polisi wilaya ya Mbinga, alisema dereva huyo amepelekwa kupatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya hiyo, akiwa chini ya ulinzi mkali.
Alisema baada ya matibabu na kupona, polisi itamhoji kufahamu chanzo cha ajali hiyo, iliyosababisha vifo na majeruhi.
Basi alilokuwa akiendesha ni lenye namba za usajili T 759 BVR, aina ya Nissan Civillian, mali ya Dismas Ndomba, mkazi wa kijiji cha Kingirikiti wilayani wilayani humo. Basi hilo lilipata ajali katika kijiji cha Burma saa 10:30 jioni Agosti mosi mwaka huu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbinga, Elisha Robert, alimwambia mwandishi, majeruhi wote ambao wamelazwa katika hospitali hiyo wanaendelea vizuri, isipokuwa wanne waliosafirishwa kwenda Hospitali ya Peramiho iliyopo Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, kutokana na kuwa katika hali mbaya.
“Vile vile tumesafirisha wagonjwa wengine wawili wameenda kupatiwa matibabu Hospitali ya Misheni Litembo iliyopo huku Mbinga, hali zao sio nzuri wamevunjika nyonga, tukaona ni vyema wapelekwe kwanza huko kwa uchunguzi zaidi wa afya zao,” alisema Dk Elisha.
Awali, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo alifafanua kwamba ajali hiyo ilisababishwa na mwendo kasi wa gari hilo.
Inadaiwa dereva wa gari hilo, alishindwa kulimudu kwenye kona kali na hatimaye lilitumbukia katika shimo kubwa na kusababisha mauaji na majeruhi hao.
Watu sita waliokufa ni Esther Kumburu ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Kilimani wilayani Mbinga. Mwingine ni Efigenia Kayombe, ambaye ni mwalimu wa shule ya Linda iliyopo Mbambabay wilayani Nyasa.
Wengine ni Ernest Ndunguru, mkazi wa kijiji cha Mikalanga wilayani Mbinga, Anna Chitete kijiji cha Kilosa wilayani Nyasa na mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Mbunda, mkazi wa kitongoji cha Lusonga Mbinga mjini na maiti ya mwanaume ambayo haikutambulika.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela amemtaja dereva huyo ni Paul Nchimbi (31), mkazi wa kijiji cha Liparamba wilayani Nyasa.
Kamanda alisema mwili wa dereva huyo, umejaa majeraha na kwa kuwa amepatikana kwa hiari yake na kuripoti katika kituo kikuu cha polisi wilaya ya Mbinga, alisema dereva huyo amepelekwa kupatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya hiyo, akiwa chini ya ulinzi mkali.
Alisema baada ya matibabu na kupona, polisi itamhoji kufahamu chanzo cha ajali hiyo, iliyosababisha vifo na majeruhi.
Basi alilokuwa akiendesha ni lenye namba za usajili T 759 BVR, aina ya Nissan Civillian, mali ya Dismas Ndomba, mkazi wa kijiji cha Kingirikiti wilayani wilayani humo. Basi hilo lilipata ajali katika kijiji cha Burma saa 10:30 jioni Agosti mosi mwaka huu.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbinga, Elisha Robert, alimwambia mwandishi, majeruhi wote ambao wamelazwa katika hospitali hiyo wanaendelea vizuri, isipokuwa wanne waliosafirishwa kwenda Hospitali ya Peramiho iliyopo Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, kutokana na kuwa katika hali mbaya.
“Vile vile tumesafirisha wagonjwa wengine wawili wameenda kupatiwa matibabu Hospitali ya Misheni Litembo iliyopo huku Mbinga, hali zao sio nzuri wamevunjika nyonga, tukaona ni vyema wapelekwe kwanza huko kwa uchunguzi zaidi wa afya zao,” alisema Dk Elisha.
Awali, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Mihayo alifafanua kwamba ajali hiyo ilisababishwa na mwendo kasi wa gari hilo.
Inadaiwa dereva wa gari hilo, alishindwa kulimudu kwenye kona kali na hatimaye lilitumbukia katika shimo kubwa na kusababisha mauaji na majeruhi hao.
Watu sita waliokufa ni Esther Kumburu ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Kilimani wilayani Mbinga. Mwingine ni Efigenia Kayombe, ambaye ni mwalimu wa shule ya Linda iliyopo Mbambabay wilayani Nyasa.
Wengine ni Ernest Ndunguru, mkazi wa kijiji cha Mikalanga wilayani Mbinga, Anna Chitete kijiji cha Kilosa wilayani Nyasa na mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Mbunda, mkazi wa kitongoji cha Lusonga Mbinga mjini na maiti ya mwanaume ambayo haikutambulika.
No comments:
Post a Comment