ANUSURIKA KUFA KWA MOTO KATIKA NYUMBA MBILI TOFAUTI



Mfanyakaziwa Benki ya NMB Tawi la Songea, alinusurika kufa na familia yake jana baada ya nyumba waliyohamia kwa muda, nayo kuteketea kwa moto.
Tukio hilo limekuja siku nne zilizopita ambapo akiwa na familia yake, walinusurika kufa baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuteketea kwa moto.
Akizungumza namwandishi ofisini kwake, juzi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Misikela alisema tukio hilo ni la Agosti 15, mwaka huu saa 5:30 asubuhi katika eneo la Msamala Manispaa ya Songea.
Kamanda alisema inadaiwa siku hiyo ya tukio, nyumba ya Maulid Mbaraka iliyopo Msamala ghafla iliungua moto, ulioanzia katika chumba kimoja kilichokuwa na vyombo mbalimbali vya Hamza Namahala na kuteketeza mali zote zilizokuwamo na thamani yake haijafahamika.
Alisema inadaiwa moto huo uligunduliwa na mtoto, Kausar Namahala (12) mwanafunzi wa shule ya mzingi Mfaranyaki, ambaye ni mdogo wa Hamza Namahala.
Mtoto huyo baada ya kugundua moto huo,  ghafla alitoa taarifa kwa majirani ambao walifika kutoa msaada. Lakini, baadaye walilazimika kutoa taarifa polisi kwa kikosi cha zima moto na walipofika eneo la tukio, walifanikiwa kuuzima licha ya kuwa baadhi ya mali zilikuwa zimeshateketea.
Kamanda Misikela alisema Namahala alipewa vyumba viwili na mfanyakazi mwenzake, Selemani Mkongo atumie kwa muda kwa kujihifadhi na familia yake baada nyumba aliyokuwa anaishi kuungua moto Agosti 12 mwaka huu. Katika tukio hilo la Agosti 12, watu watatu wa familia hiyo walizimia na kulazwa hospitali ya Mkoa kwa matibabu.

No comments: