Taasisi
ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) inatarajia kudahili
wanafunzi takribani 400 kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo, yanayotarajia kuanza
Agosti mwaka huu.
Akizungumza juzi Ofisa Mawasiliano wa taasisi
hiyo, Scholastica Njozi alisema udahili huo utakuwa ni kundi la 17 la kupata
mafunzo kwa vitendo tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo miaka mitano iliyopita.
“ Hadi Juni mwaka huu, tumeshadahili makundi
kumi na sita na kupata mafunzo na wengine bado wanaendelea na mafunzo,”
alisema.
Taasisi imedahili jumla ya wanafunzi 4,189,
wanafunzi 1,107 kati yao bado wanaendelea na mafunzo, wanafunzi 3,082
wamemaliza mafunzo na kufanya mitihai ya Taasisi. Kati ya waliomaliza wanafunzi
1,445 wamefaulu mitihani yote na kupewa tuzo ya stashahada ya uzamili katika
utaalamu wa kisheria.
Tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo, wahitimu
wote wa shahada ya sheria kutoka vyuo vinavyotambuliwa na serikali na vyuo
binafsi, wanaotarajia kufanya kazi kama mawakili binafsi nchini au katika
utumishi wa umma, hufanya mafunzo ya mwaka mmoja katika taasisi hiyo na kufaulu
mitihani.
Njozi alisema lengo la kuanzishwa kwa taasisi
hiyo, ni kuhakikisha haki inamfikia kila Mtanzania na kwa wakati, kwa kuwa
mafunzo hayo yanaboresha stadi, ujuzi na viwango vya utendaji kazi wa wanasheria
nchini.
No comments:
Post a Comment