Waendesha
pikipiki, maarufu ‘Bodaboda’ wameshauriwa kununua vifaa sahihi kwa ajili ya
vyombo hivyo ili kuepuka madhara yanayoweza kuwatokea pindi wakitoa huduma ya
usafiri.
Ushauri
huo ulitolewa jana jijini hapa na Meneja Masoko, Kanda ya Afrika kutoka Kampuni
ya Mek-one General Traders, Benard Kituyi wakati akitambulisha mafuta ya Shell
Advance mahususi kwa pikipiki.
Alisema
baadhi ya wamiliki na madereva wa bodaboda hushindwa kununua vifaa sahihi kwa
ajili ya pikipiki zao jambo ambalo husababisha wakati mwingine kutokea tatizo
ambalo lingeweza kudhibitiwa mapema.
“Unapotumia
vifaa ambavyo si mahususi kwa pikipiki ni wazi kwamba unafanya usafiri husika
kupokea kitu ambacho si sahihi kwake na hivyo kulazimisha jambo ambalo ni
hatari kwa vifaa vya moto,”alisema Katuyi.
Alisema
katika kuhakikisha huduma ya usafiri wa pikipiki inakuwa salama, kampuni hiyo
ina mpango wa kukutana na waendesha bodaboda 30,000 ambao watawaelimisha
umuhimu wa kutumia mafuta hayo na namna ya kutumia barabara kwa njia
salama.
“Mafunzo
hayo yatatolewa kwa wiki moja kuanzia leo (jana) yakiambatana na kutoa vifaa
kama makoti maalum ‘reflect jacket’ ya kuvaa ambayo yatawasaidia kuonekana
wawapo barabarani, hivyo kuwakinga na ajali,” alisema.
Alisema
kwa kuanzia mafunzo hayo yataanzia Dar es Salaam yakifuatiwa na Arusha, Mbeya
na mikoa mingine ambayo wanaamini usafiri huo unatumiwa kwa wingi na watu.
Kwa
upande wake mmoja wa waendesha bodaboda, Razaki Juma, alizishukuru kampuni hizo
kwa kujitoa kuwapa elimu ya namna ya kutumia mafuta kwani awali walikuwa
hawajui matumizi ya mafuta ya magari kama ndio yanachangia kila siku kupeleka
pikipiki zao kwa mafundi.
No comments:
Post a Comment