VODACOM YAANDAA GULIO LA WAZI LEADERS CLUB

Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania imeandaa gulio la wazi kwa ajili ya mauzo ya bidhaa mbalimbali, ikiwemo simu na ipad kuwezesha umma kupata bidhaa hizo kwa gharama nafuu. 
Gulio hilo maarufu kwa jina la Vodacom Expo linalotarajiwa kufanyika kwa siku mbili mfululizo kuanzia Juni 28, litakuwa katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni.
Meneja Uhusiano wa Nje wa kampuni hiyo, Salum Mwalim alisema wanatarajia kuuza bidhaa hizo kwa bei ya chini tofauti na ya soko. 
"Mwaka jana kwa mara ya kwanza tulipoitisha gulio hili tulishuhudia idadi kubwa ya watu wakifurika kwa ajili ya kupata bidhaa mbalimbali za simu za mkononi, hali hiyo ilitupatia ujumbe kuwa wazo tulilolibuni limepokelewa vema na Watanzania,” alisema Mwalim. 
Alisisitiza lengo la kampuni ni kuhakikisha wananchi wanakuwa na uwezo wa kumiliki simu bora na ya kisasa kwa ajili ya mawasiliano ya sauti na huduma za intaneti. 

No comments: