Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, Kilimuka Garigunga anataka dagaa ambao wamepewa jina la ‘dagaa wa Kigoma’ kubadilishwa na kuitwa wa Nkasi kwa kile alichodai wanavuliwa zaidi wilayani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni ofisini kwake, alisema dagaa hao wavuliwao Ziwa Tanganyika, wanapatikana zaidi wilayani kwake kuliko mkoani Kigoma.
Kwa mujibu wake, Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Nkasi lina ukubwa wa kilometa za mraba 3,749 ukiwa na ukanda wenye urefu wa kilometa 130.
Takwimu za makadirio ya Sensa ya Uvuvi iliyofanyika 2010-11 zinaonesha kuwa eneo la Ziwa Tanganyika upande wa Wilaya ya Nkasi lina uwezo wa kuvuliwa tani 4,911 za aina mbalimbali za samaki wakiwemo dagaa wenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 7.0 kwa mwaka.
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni ofisini kwake, alisema dagaa hao wavuliwao Ziwa Tanganyika, wanapatikana zaidi wilayani kwake kuliko mkoani Kigoma.
Kwa mujibu wake, Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Nkasi lina ukubwa wa kilometa za mraba 3,749 ukiwa na ukanda wenye urefu wa kilometa 130.
Takwimu za makadirio ya Sensa ya Uvuvi iliyofanyika 2010-11 zinaonesha kuwa eneo la Ziwa Tanganyika upande wa Wilaya ya Nkasi lina uwezo wa kuvuliwa tani 4,911 za aina mbalimbali za samaki wakiwemo dagaa wenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 7.0 kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment