Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kupitia Baraza
la Taifa la Elimu ya Ufundi ( NACTE),
imefungua ofisi tano za kanda,
ikiwa ni sehemu ya mkakati wa wizara ya kuwekeza katika eneo la
usimamizi wa sekta ya elimu nchini kuongeza ufanisi na kufikia Matokeo Makubwa
Sasa (BRN).
Ofizi hizo na makao yake makuu kwenye mabano
ni Kanda ya Kaskazini (Arusha), Kanda ya Ziwa (Mwanza), Kanda ya Kusini (Mbeya), Kanda ya Kati
(Dodoma) na Zanzibar.
Katika uzinduzi wa kanda hizo, uliofanyika
mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni
Mchome alisema kanda hizo zitaongeza
ufanisi na usimamizi wa elimu ya ufundi nchini.
Alisema Wizara itaendelea kutekeleza mikakati iliyojiwekea kuhakikisha ubora wa elimu unasimamiwa vema
na unalindwa hiyo ikiwa ni pamoja na kukabili watoa huduma kwenye sekta ya
elimu wasiokuwa makini.
Alisema utamaduni wa kutegemea ofisi zilizopo
makao makuu Dar es Salaam, unapaswa
kurekebishwa kuwawezesha wananchi kupata
huduma katika sekta ya elimu kwa ukaribu zaidi jambo ambalo litawapunguzia pia
gharama
Mkurugenzi Mtendaji wa NACTE , Dk Primus
Nkwera alisema ofisi hizo za kanda, zitakuwa na majukumu ya kusimamia na
kutekeleza mipango na mikakati ya Baraza na Wizara kwa ujumla katika sekta ya
elimu ya ufundi nchini ikiwemo udhibiti na usimamizi wa vyuo vya elimu ya
ufundi.
No comments:
Post a Comment