Mfanyakazi
wa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo, Obedi Laiser ameibuka kidedea katika
shindano la kumtafuta mfanyakazi bora lililoshirikisha wafanyakazi 21 kutoka
nchi mbalimbali za Afrika na Marekani ya Kusini.
Amesema
ushindi huo kwa hakika si wa kwake au Kampuni ya Tigo pekee bali ni kwa Taifa
zima la Tanzania na anajivunia hilo.
Shindano
hilo lililofanyika Marekani wiki iliyopita, liliwahusu wafanyakazi kutoka nchi
zenye huduma ya mawasiliano chini ya Kampuni ya Mawasiliano na Vyombo vya
Habari ya Uswisi ya Millicom. Kampuni hiyo ambayo Tigo ipo chini yake, ndio
iliandaa shindano hilo.
Laizer
akiwa mmoja kati ya washindani 21 waliochaguliwa kutoka nchi mbalimbali,
alisema kuwa ushindi huo si wake tu bali ni wa Taifa kwa ujumla.
Alisema
kuwa ushindi huo unatoa taswira nzuri kuwa Watanzania ni watu wa kuchapa kazi
na wanaweza kuwakilisha vema sehemu mbalimbali.
"Haya
ni mashindano yaliyoshirikisha wafanyakazi kutoka nchi mbalimbali ambazo
zinahuduma za kampuni hiyo ya mawasiliano ya kidigitali ya Millicom sasa kwa
hapa Tanzania mimi niliwakilisha nikitokea Tigo na ndio nimeshinda,"
alisema Laizer.
Laizer
aliteuliwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez kushiriki katika
shindano hilo akiwakilisha Tanzania kutokana na ufanyaji wake wa kazi kwa
nidhamu.
Gutierrez
akizungumzia ushindi huo alisema kuwa hata akiwa katika utendaji wake wa kazi
wa kila siku ni mtu mwenye mtazamo chanya katika kila kazi anayoifanya na
amestahili tuzo hiyo.
"Ni heshima kwa nchi nzima
kutambuliwa kama hivi kutoka Millicom, ambaye ni kiongozi wa ulimwengu
katika kutoa maisha ya kidigitali na huyu kijana ametoa picha nzuri kwa vijana
wengine wa Kitanzania kuwa kumbe wanaweza kufanya kazi zao vema," alisema
Gutierrez.
No comments:
Post a Comment