Maofisa Elimu wawili wa Manispaa ya Tabora na
Ofisa Utamaduni, wamefikishwa kujibu mashitaka mawili ya kuhujumu uchumi.
Waliofikishwa mahakamani ni Ofisa Elimu
Taaluma, Rajab Kiteu, Ofisa Elimu Ufundi, Maiko Sawasawa na Ofisa
Utamaduni, Madereko Katunzi.
Walifikishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi
Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Tabora, Issa Magoli.
Upande wa mashitaka ukiongozwa na Simon
Mashingia kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) alidai
maofisa hao walitenda makosa hayo Julai mwaka 2011.
Katika shitaka la kwanza, ilidaiwa watuhumiwa
wote kwa pamoja wakiwa ni watumishi wa Manispaa ya Tabora, kwa kutumia nyaraka,
walimdanganya mwajiri kitendo ambacho ni kosa kinyume na sheria.
Katika shitaka lingine, Mwendesha Mashitaka
alidai kila mmoja alimwibia mwajiri Sh 955,000.
Wote walikana mashitaka hayo na wako nje kwa
dhamana hadi Julai 15 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.
No comments:
Post a Comment