Madereva watatu wa bodaboda wamekufa
katika matukio matatu tofauti yaliyohusisha ajali za barabarani.
Katika tukio la kwanza, Ally Omary
(29) amekufa papo hapo na abiria wake kupata majeraha baada ya kugongana na
gari la kijeshi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni,
Camillius Wambura alisema tukio hilo lilitokea juzi, saa 8:30 mchana katika
barabara ya New Bagamoyo maeneo ya lango kuu Lugalo Jeshini, Wilaya ya
Kinondoni.
Alisema gari la kijeshi aina ya
Iveco ambalo halikufahamika namba ya gari hilo na dereva wake, ilitoka upande
wa barabara ya Lugalo Jeshini Hospitali na kwenda upande wa pili katika njia
isiyoruhusiwa na kugongana na pikipiki yenye namba za usajili T 956 BAH aina ya
Skymark.
Alisema dereva huyo wa pikipiki alimpakia abiria aitwaye Ridhiwani Waziri na kwamba pikipiki hiyo ilitokea Mwenge kuelekea njia panda ya Kawe ndipo lori hilo la jeshi lilikatiza mbele yake na kushindwa kuzuia pikipiki hiyo.
Kwa mujibu wa Wambura, dereva wa gari la jeshi alikimbia na gari lake. Majeruhi amelazwa katika Hospitali ya Lugalo Jeshini na maiti amehifadhiwa hospitalini hapo.
Alisema dereva huyo wa pikipiki alimpakia abiria aitwaye Ridhiwani Waziri na kwamba pikipiki hiyo ilitokea Mwenge kuelekea njia panda ya Kawe ndipo lori hilo la jeshi lilikatiza mbele yake na kushindwa kuzuia pikipiki hiyo.
Kwa mujibu wa Wambura, dereva wa gari la jeshi alikimbia na gari lake. Majeruhi amelazwa katika Hospitali ya Lugalo Jeshini na maiti amehifadhiwa hospitalini hapo.
Alisema chanzo cha ajali hiyo ni
uzembe wa dereva wa gari la jeshi kukatiza barabara kwa kutumia njia
isiyoruhusiwa.
Wakati huo huo, Abdallah Seif (30)
amekufa papo hapo baada ya pikipiki yake kugongwa kwa nyuma na gari
lisilofahamika.
Wambura alisema ajali hiyo ilitokea
jana saa 8:03 usiku katika barabara ya Morogoro eneo la mataa Magomeni Wilaya
ya Kinondoni.
Alisema gari ambalo halikufahamika
lilikuwa likitokea Ubungo kuelekea Kariakoo likiwa na uelekeo sawa na pikipiki
yenye namba za usajili T 439 CHU aina ya Fekon iliyokuwa ikiendeshewa na
Seif na kusababisha kifo chake. Maiti amehifadhiwa katika Hospitali ya
Taifa ya Muhimbili.
Katika tukio la tatu, dereva wa
pikipiki, Ismail Shengwatu (25) mkazi wa Ukonga amekufa baada ya kugongwa na
gari.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala,
Marietha Minangi alisema ajali hiyo ilitokea juzi saa 3:30 usiku katika
barabara ya Mandela maeneo ya Sukita Wilaya ya Ilala.
Alisema gari lenye namba za usajili
T 457 AGR aina ya Trailer likiwa na gari lenye namba za usajili T 505 AHD
aina ya Scania likitokea njia panda ya Tabata kuelekea Buguruni
uelekeo mmoja na pikipiki yenye namba za usajili T 940 CBG aina ya Boxer.
Alisema dereva wa pikipiki hiyo
alijaribu kupita lori T 505 AHD na ghafla mbele yake alikutana na gari
lililokuwa limeharibika bila ya tahadhari, alijaribu kurudi upande wa kushoto
ndipo aligonga Trailer na kufa papo hapo.
Maiti amehifadhiwa katika Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili na upelelezi unaendelea.
No comments:
Post a Comment