Jamaa
mmoja kutoka kijijini alitumwa kuja Dar kufuatilia hali ya baba yake aliyekuwa
amelazwa katika Hospitali ya Muhimbili. Alipofika akapigiwa simu na wenzake wa
kijijini na mambo yakawa hivi. JAMAA: Haloo nimefika salama na tayari nimeshamuona
mgonjwa wetu. KIJIJINI: Enhe, hali yake vipi? JAMAA: Anaendelea vizuri kabisa,
afya yake imeniridhisha mno. KIJIJINI: Amelazwa wodi gani? JAMAA: Wodi
aliyokuwa mwanzo siikumbuki vizuri, nakumbuka hii aliyohamishiwa sasa.
KIJIJINI: Wodi gani hiyo? JAMAA: Nakumbuka mlangoni ilikuwa imeandikwa
Mochwari!! Duh, kasheshe…
No comments:
Post a Comment