Wizara
ya Kilimo, Chakula na Ushirika imewaomba wadau wa sekta ya sukari nchini
wakiwemo wazalishaji katika viwanda vya ndani kuendelea kutoa
ushirikiano
wa karibu na vyombo vya dola kwa kuhakikisha wanawafichua
wafanyabiashara wasio waaminifu wanaoingiza sukari kwa njia ya
magendo.
Kauli
hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo , Godfrey Zambi,
wakati akizungumza na Menejimeti ya Kiwanda cha Sukari Kilombero , juzi.
Naibu
huyo alifanya ziara ya kuangalia hali ya uzalishaji wa sukari na kupata
changamoto kutoka kwa Uongozi wa kiwanda hicho.
Hata
hivyo alisema, licha ya viwanda vya ndani kutokuwa na uwezo wa
kukidhi mahitaji ya sukari nchini, na kuifanya Serikali kulazimika kuziba
pengo
hilo kwa kuagiza sukari toka nje , hatua hiyo isitumike visivyo na
wafanyabiashara hao kwa kukiuka utaratibu uliowekwa kisheria.
“
Katika kudhibiti jambo hilo ,TRA imepewa kazi hiyo
kuona
na kuhakikisha sukari inayoingia kwa magendo
inadhibitiwa
na pia inayosafirishwa inakuwa chini ya uangalizi maeneo yote” alisema Naibu
Waziri.
Kwa
mujibu wa Naibu Waziri huyo, TRA pia imepewa jukumu la kupitia upya sheria ya
kodi kwa bidhaa hiyo inayoagizwa kutoka nje ili bei yake isiweze
kuathiri
ushindani wa soko kutoka viwanda vya hapa nchini.
Kwa
upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Sukari Kilombero,
Joseph Rugaikamu alitoa taarifa ya hali ya uzalishaji wa sukari
kwenye kiwanda hicho alisema hadi kufikia Mei 17, mwaka huu kilikuwa na
tani za sukari 24,999 zilizokosa soko.
Naye
Meneja Maendeleo Mipango na Uratibu wa Bodi ya Sukari nchini, Abdul Mwamkemwa
,alisema katika kudhibiti uingizaji wa sukari na magendo na kutolipiwa
kodi , Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA ), ndio wenye jukumu la
kusimamia na tayari wamebuni njia mbadala ya kudhibiti hali hiyo ambayo
itaondoa hali inayojitokeza kwa sasa.
No comments:
Post a Comment