Watu watano wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Ilala, kujibu mashitaka ya kuvunja msikiti.
Watu hao ni Mohamed Ngwai (31), Issa Karim(40), David Kambarage (32), Melkiori Utoh (33)na Athuman Msagati (30).Wakili wa Serikali, Ester Kyala alidai mbele ya Hakimu John Msafiri kuwa Mei 2 mwaka huu eneo la Zanaki Wilaya ya Ilala, washitakiwa hao walivunja msikiti wa Satan Zamra.
Washitakiwa walikana mashitaka. Kati ya hao, Ngwai na Utoh waliachiwa huru baada ya kutimiza masharti ya dhamana.
Hakimu Msafiri aliwataka kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa, watakaosaini kulipa Sh milioni moja.
Wakati huo huo, mkazi wa Mwananyamala Kisiwani amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Ilala, kujibu mashitaka ya wizi wa kutumia silaha.
No comments:
Post a Comment