Chuo cha Ufundi Arusha kimefanikiwa
kuwajengea uwezo wa kujiamini wasichana zaidi ya 1,498 kwa kuwapatia programu
mbalimbali za ufundi.
Wamepewa mafunzo hayo katika kipindi
cha miaka mitano iliyopita. Mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha
wasichana wengi wanaingia katika soko la ajira.
Katika mafunzo hayo, wamejengewa uwezo
katika fani za uhandisi ufundi, uhandisi umwagiliaji, ufundi magari, ufundi
umeme na programu nyingine zinazoendeshwa na chuo hicho.
Hayo yameelezwa na Mhadhiri Msaidizi katika Idara ya
Umwagiliaji chuoni hapo, Dk Nuru Mziray.
Alisema chuo kinahakikisha wanafunzi wa
kike kuanzia msingi na sekondari, wanahamasishwa kusoma masomo ya sayansi
kuanzia mwanzo.
Pia alisema chuo hicho kimekuwa kikiwafuatilia
maendeleo yao mpaka wanapomaliza elimu ya msingi ama sekondari na kuwasisitizia
umuhimu wa masomo ya sayansi na teknolojia kwao.
Mziray alisema Tanzania idadi ya
wasichana wanaoamua kusoma masomo ya sayansi wakiwa katika shule za sekondari
na vyuoni ni ndogo mno.
Alisema katika mwaka ujao wa masomo,
chuo kimepanga kuchukua wasichana 411 wa fani mbalimbali.
No comments:
Post a Comment