Ranchi
ya Taifa ya Kongwa (Narco) iliyoko wilayani Kongwa mkoani Dodoma,
imevamiwa na wanavijiji ambao wamefanya uharibifu mkubwa katika eneo la hifadhi
yake.
Pamoja
na uharibifu wa hifadhi yake, wananchi hao wamekuwa wakiiba na kuua baadhi ya
mifugo na kujeruhi.
Kauli
hiyo imetolewa na Meneja wa Ranchi ya Taifa Mwandamizi Heslon Kashalankolo
wakati akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki waliotembelea
hifadhi hiyo.
Meneja
huyo alisema ranchi hiyo imeharibiwa kwa asilimia 70 kutokana na wananchi
kuvamia na kulima mashamba makubwa yakiwemo ya mahindi ndani ya hifadhi.
Aliongeza
kuwa hata maisha ya wafanyakazi wa ranchi hiyo yako mashakani kutokana na wengi
wao kuvamiwa na wananchi hao wakiwa machungani na kuporwa ng’ombe huku baadhi
yao wakiuawa na kufukiwa na wananchi hao ili kupoteza ushahidi.
Alisema
mwaka jana kuna mfanyakazi wao mmoja aliuawa akiwa machungani na kumzika
porini, ambapo baada ya kutomwona kwa siku tatu waliamua kumtafuta na ndipo
walipokuta kaburi lake porini.
“Kwa
kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2013, ranchi imepoteza
wafanyakazi wake watatu kwa kuuawa na wananchi wakiwa machungani na wengine 16
wamejeruhiwa kwenye majaribio mbalimbali ya wizi wa ng’ombe,” alisema
Kashalankolo.
Kwa
upande wake mbunge wa Longido, Michael Laizer, alipotembelea ranchi hiyo na
kujionea uharibifu mkubwa wa mazingira uliofanyika aliitaka Serikali
kuumaliza mgogoro huo kwani upo ndani ya uwezo wake.
Ranchi
hiyo ya Taifa ilianzishwa mwaka 1948 ambapo ina ukubwa wa hekta 38,000 na
mifugo 8,000 wakiwemo ng’ombe, farasi, mbuzi na kondoo ambao hufugwa kisasa.
No comments:
Post a Comment