WANAOWATUKANA WAASISI WA MUUNGANO WASHITAKIWE



Serikali imetakiwa kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wote wanaotoa matusi na kuwakashifu waasisi wa Muungano wa Tanzania ili kukomesha vitendo
hivyo visijirudie tena.
Mmoja wa wakimbiza Mwenge Kitaifa, Wito Mlemelwa alizungumza hayo  wakati akiwaaga viongozi wa Mkoa Kigoma ili kuendelea na mbio za Mwenge
mkoani Katavi.
Mlemelwa alisema kuwa katika mchakato wa Katiba mpya unaoendelea kumekuwa na matusi na maneno ya kashfa kwa waasisi wa Muungano lakini wale wote waliofanya hivyo hawajachukuliwa hatua yoyote na kwamba wakati umefika sasa wa jambo hilo kutovumiliwa na hatua zinazostahili zichukuliwe.
Mkimbiza Mwenge huyo alisema kuwa kama mtaani watu wa chini wakitukanwa wanakamatwa na kuchukuliwa hatua kwa kuwekwa rumande kwa nini hao wanaotukana na kutoa kashfa hadharani wasichukuliwe hatua, ametaka sheria ambayo ni msumeno kufanya kazi yake sawa sawa na kwa uwiano.
Awali Mkuu wa Mkoa Kigoma Issa Machibya alisema kuwa Serikali haitakubali kikundi cha watu wachache kuvuruga amani na utulivu miongoni mwa Watanzania
kwa ajili ya maslahi yao wakati wa mchakato wa Katiba mpya.

No comments: