Vyama
10 vya siasa kati ya 21 vyenye usajili wa kudumu, vimeshindwa kuwasilisha
hesabu zao za vyama kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa
ajili ya ukaguzi.Kati ya hivyo, vyama 11 havikuwasilisha taarifa zao huku vinne
vilivyokaguliwa havina akaunti ya benki.Hayo yalielezwa jana na Mkaguzi na
Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari jana mjini hapa na kuongeza kuwa hakuna chama cha siasa
kilichowasilisha tamko la mali zinazomilikiwa na chama.Kwa mujibu wa Utouh,
mpaka sasa hakuna chama cha siasa kilichowasilisha
kwa Msajili wa Vyama vya Siasa tamko la mali zinazomilikiwa na chama
husika.Alisema katika ukaguzi huo, alikutana na changamoto nyingi katika
ukaguzi wa fedha ambazo si za umma.Mkaguzi huyo alivitaja vyama ambavyo havina
akaunti ya benki kuwa ni pamoja na UMD, NLD, NRA na ADC.Alisema kwa sasa
utaratibu unafanyika ili kuangalia upya utaratibu wa sheria ya Msajili wa Vyama
vya Siasa, ili kuwezesha vyama hivyo kukaguliwa.
“Kuna
baadhi ya vyama havina ruzuku hivyo wakati mwingine unaweza kupata changamoto,’’
alisema.
Akizungumzia
hali ya magereza hapa nchini, alisema hivi sasa kuna magereza 122 hapa nchini.
Alisema
magereza hayo kwa sasa yanatoa huduma kwa wafungwa 45,000 wakati uwezo wake ni
wafungwa 22,669.‘’
Hali
hii imeongeza ugumu wa udhibiti na kufuatilia haki za wafungwa kwenye magereza
yenye msongamano mkubwa kiasi hicho,’’ alisema.
CAG
alisema katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2013 jumla ya hati 961 za ukaguzi zilitolewa (bila
kujumuisha kaguzi maalum 16 na za ufanisi sita ).
Alisema
kati ya hati hizo, hati zinazoridhisha ni 816 ambazo ni sawa na asilimia 85,
hati za shaka ni 131 sawa na asilimia 13.6, hati zisizoridhisha ni nane sawa na
asilimia 0.8 na hati mbaya sita sawa na asilimia 0.6.
“Pamoja
na kwamba kuna jumla ya hati mbaya sita na hati zisizoridhisha nane kwa taasisi
zote nilizokagua kwa mwaka huu, mwelekeo wa hati za ukaguzi kwa ujumla
unaonesha kuimarika kwa utendaji wa Serikali katika kusimamia makusanyo ya
mapato na matumizi,” alisema.
Pia
alisema kwa mwaka ulioishia Juni 30, mwaka huu hali ya deni la taifa lilifikia
kiasi cha Sh trilioni 21.2, ongezeko la trilioni 4.2 sawa na asilimia 25
ikilinganishwa na kiasi cha Sh trilioni 16.9 mwaka 2011/2012 deni hilo
linajumuisha deni la ndani na deni la nje.
Alisema
hali halisi ya deni la ndani lilifika kiasi cha Sh. trilioni 5.7 kwa mwaka
ulioishia Juni 30, mwaka huu ikiwa ni ongezeko la trilioni 1.2 sawa na asilimia
27 kutoka kiasi cha trilioni 4.5 kwa mwaka 2011/01.
Utouh
alisema ongezeko hilo lilisababishwa na mikopo kutoka kwa mabenki na wafadhili
wa nje, kwa ajili ya kusaidia miradi mikubwa ya maendeleo kama uboreshaji wa
miundombinu katika nyanja za usafirishaji, majisafi, mkongo wa mawasilino wa
Taifa na bomba la gesi.
Alisema
taarifa za misamaha ya kodi kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2013 zimeonesha kiasi
cha Sh trilioni 1.5 kilitolewa kama misamaha ya kodi.
Hata
hivyo, alisema misamaha ya kodi kwa mwaka ulioishia Juni 30, mwaka 2013
imepungua kutoka Sh trilioni 1.8 mwaka 2011/2012 hadi trilioni 1.5 mwaka
2012/013.
“Ukaguzi
wangu pia umebaini mishahara kwa watumishi walioacha kazi, waliofariki,
waliostaafu imeendelea kulipwa kupitia
katika akaunti zao,” alisema.
Alisema Sh bilioni 1.6 na makato ya Sh milioni 497
ziliendelea kupelekwa kwenye taasisi kama Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa, Mamlaka
ya Mapato na Mifuko ya Jamii.
Pamoja
na hayo, Utouh alitaka serikali kuangalia namna ya kuwekeza katika majengo yake
yenyewe kwani ukaguzi ulibaini ofisi 14 za Serikali zililipwa Sh bilioni 7.9 za kodi ya pango kwa mwaka.
No comments:
Post a Comment