Vijiji
vitano wilayani Kilwa katika Mkoa wa Lindi vilivyo kwenye mpango maalumu wa
kusafirisha na kuuza magogo nje ya nchi, vimejipatia zaidi ya Sh milioni 203
kati ya mwaka jana na mwaka huu kutokana na mauzo hayo .
Mshauri
wa Masuala ya Mawasiliano katika mradi wa kuhifadhi na kuendeleza misitu ya
asili, Abigail Wills alisema vijiji vya Kisangi, Liwiti na Nanjilinji A
vinapeleka magogo ya asili hasa Mpingo kwa watengenezaji wa vifaa vya muziki
nchini Uingereza na nchi nyingine za Ulaya.
"Novemba
mwaka jana tuliongeza kijiji kingine kiitwacho Likawage chenye msitu wa asili
wenye ukubwa wa hekta 17,921" alisema Wills.
Kijiji
cha Kikole kilichoingia kwenye mpango huo mwaka 2009 kimejipatia Sh
milioni 10. Aidha kijiji kilichonufaika zaidi ni Nanjilinji A kilicho na eneo
la hekta 61,505 baada ya mauzo kilipata Sh milioni 112.5.
No comments:
Post a Comment