VIFAA VYA KISASA VYAKWAMISHA UPIMAJI HALI YA HEWA



Ukosefu wa vifaa vya kisasa vya kupimia hali ya hewa katika nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania, umesababisha nchi hizo kushindwa kukabiliana na changamoto za ongezeko la mabadiliko ya hali ya hewa na tabia nchi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Agness Kijazi, alisema hayo wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa kitaifa kuhusu mpango wa mashauriano kwa ajili ya huduma za hali ya hewa barani Afrika.
Mpango huo umefadhiliwa na Serikali ya Norway, kwa ajili ya   kuanzishwa kwa huduma ya hali ya hewa ya kusaidia nchi za Afrika, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuongeza hali ya kupambana na ukame na mafuriko ya mara kwa mara.
Akizungumza kwa Niaba ya Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Dk Kijazi alisema kuna umuhimu  wa wananchi kutumia taarifa za TMA kwa ajili ya maisha yao ya kila siku.
Alisema hata wakulima wanatakiwa kufuatilia taarifa hizo kwa ukaribu zaidi, ili kujua mazao wanayostahili kulima kutokana na hali ya hewa.

No comments: