Wazee
wawili akiwemo mlinzi mmoja wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya wilaya ya
Bunda, mkoani Mara, wamefikishwa mahakamani kwa kosa la kulawiti wanafunzi sita
wa shule za msingi zilizoko wilayani hapa.
Waliofikishwa
katika Mahakama ya Wilaya ya Bunda, ni pamoja na Thomas Machugu (72) ambaye ni
mlinzi na mkazi wa mtaa wa Saranga,
mjini hapa.
Mwingine
ni Salum Mfumbasi (66) ambaye ni mfanyakazi wa ndani kwa mfanyabiashara mmoja
wa mjini Bunda.
Watuhumiwa
hao walifikishwa jana katika mahakama hiyo mbele ya hakimu, James Manota na
kusomewa mashitaka yao na mwendesha mashitaka wa polisi Masood Mohammed.
Akiwasomea
mashitaka yao, Mohammed alisema washitakiwa hao wote kwa pamoja waliwalawiti
wanafunzi hao, ambao umri wao ni kati ya miaka 10 na 13 kwa tarehe na muda
tofauti, katika maeneo mbalimbali mjini hapa.
Alisema
kuwa polisi waliwagundua watu hao baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema
na kwamba baada ya kuwahoji watoto hao walisema kila kitu jinsi washitakiwa hao
wamekuwa wakiwaingilia kwa zamu, pindi wanapokwenda shuleni baada ya kupita
katika maeneo hayo.
Aidha,
aliongeza kuwa baada ya watoto hao kupelekwa hospitalini na kufanyiwa uchunguzi
wa kitabibu ilibainika kuwa walikuwa wamekwishaharibiwa sehemu zao za siri.
Washitakiwa
wote kwa pamoja wamekana mashitaka yao na kupelekwa mahabusu hadi Mei 22 mwaka
huu, kesi yao itakapotajwa tena mahakamani hapo.
No comments:
Post a Comment