Utekelezaji
wa mkakati wa Matokeo Makubwa Sasa katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),
umeelezwa kwenda vizuri.
Ripoti
iliyotolewa hivi karibuni na TPA ya kati ya Julai 2013 na Machi 2014 kuhusu
utekelezaji wa mkakati huo, imeonesha pamekuwa na maendeleo makubwa na
kuongezeka kwa ufanisi katika Bandari ya Dar es Salaam, ikilinganishwa na kabla
ya Julai mwaka jana.
Pamoja
na mambo mengine, mkakati wa Matokeo Makubwa Sasa unalenga kubadilisha bandari
za Tanzania na hasa ile ya Dar es Salaam kuwa kitovu kikuu cha uchumi Tanzania
na kutoa ushindani katika ukanda wa Afrika.
Kwa
mujibu wa ripoti hiyo, pamekuwa na ongezeko la mizigo katika bandari hiyo kwa
muda huo unaofikia tani milioni 10.95, ikiwa ni mafanikio kwa asilimia 84.2
kabla ya kufikia lengo la tani milioni 13 kwa
mwaka 2013/2014.
Muda
wa meli kukaa bandarini kwa mwezi Machi mwaka huu, ilikuwa siku 6.1 kwa meli,
mafanikio ya asilimia 82.0 kabla ya kufikia lengo la siku 5 kwa
meli.
Kwa
mujibu wa ripoti hiyo, muda wa kukaa kwa mizigo bandarini kutoka nje kwa Machi
mwaka huu, ilikuwa siku 10.0 kwa kontena, ikilinganishwa na lengo la siku 7 kwa
kontena.
“Hali
hii imesababishwa na miundombinu mibovu ya reli na kutegemea usafirishaji kwa
njia ya barabara kwa kiwango kikubwa,” imeeleza ripoti hiyo.
Uwezo
wa kutoa magari bandarini, umeongezeka kwa asilimia 100.7 kwa mwezi Machi mwaka
huu, na magari 604 yakitolewa kwa awamu.
Ripoti hiyo ilisema kuwa kwa Machi 2014, lengo la kutumia siku tatu kwa lori moja la
mizigo kuwa limeondoka bandarini, limefikiwa kwa asilimia 81.1, kwani sasa lori
moja linatumia siku 3.3.
No comments:
Post a Comment